NABII TITO AMETHIBITIKA KUWA NA MATATIZO YA AKILI.

Mtu aliyezua gumzo hivi karibuni kwa kujiita nabii Tito, ambaye jina lake halisi ni Onesmo Machija, mwenye umri wa miaka 44 amepelekwa hospitali ya Mirembe Dodoma  kwa ajili ya matibabu ya akili.

Hii ni baada ya kubainika kuwa mtu huyo ana matatizo ya akili kupita mahojiano baina yake na jeshi la polisi mkoani Dodoma.
Hayo yamebainishwa na kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Dodoma Gillesi Muroto wakati akizungumza na wanahabari.

Kamanda Muroto amefafanua kuwa, mnamo tarehe 23 Juni 2014 mtu huyo alilazwa hosipitali ya taifa ya muhimbili kwaajili ya matibabu ya akili, ambapokwa mujibu wa taarifa za  kidaktari alipaswa kurejea hosipitalini hapo tarehe 9 mwezi Julai mwaka huohuo lakini hakurejea, na matokeo yake hivi karibuni aliibuka katika kijiji cha Nghong'ona kilichopo jirani na chuo kikuu cha Dodoma (UDOM) na kuendesha mahubiri ya kidini yasiyozingatia maadili huku kanisa lake likiwa halitambuliki.

Kufuatia hali hiyo Jeshi la polisi lilimshikilia na kufanya mahojiano naye na ndipo ilipobainika kuwa mtu huyo ana matatizo yaakili  na hatimaye alifikishwa katika hosipitali ya rufaa ya Mirembe iliyoko mjini Dodoma kwaajili ya uchunguzi ambapo Daktari Dixon Philipo baada ya kumfanyia vipimo alitoa uthibitisho kuwa mtu huyo bado ana matatizo ya akili.



Comments